Psalms 135:1-6
Wimbo Wa Sifa Kwa Mungu
1 aMsifuni Bwana.
Lisifuni jina la Bwana,
msifuni, enyi watumishi wa Bwana,
2 bninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana,
katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3 cMsifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema,
liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.
4 dKwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe,
Israeli kuwa mali yake ya thamani.
5 eNinajua ya kuwa Bwana ni mkuu,
kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.
6 f Bwana hufanya lolote apendalo,
mbinguni na duniani,
katika bahari na vilindi vyake vyote.
Copyright information for
SwhKC