Psalms 135:1-6

Wimbo Wa Sifa Kwa Mungu


1 aMsifuni Bwana.

Lisifuni jina la Bwana,
msifuni, enyi watumishi wa Bwana,

2 bninyi ambao mnatumika ndani ya nyumba ya Bwana,
katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.


3 cMsifuni Bwana, kwa kuwa Bwana ni mwema,
liimbieni sifa jina lake, kwa maana hilo lapendeza.

4 dKwa maana Bwana amemchagua Yakobo kuwa wake mwenyewe,
Israeli kuwa mali yake ya thamani.


5 eNinajua ya kuwa Bwana ni mkuu,
kwamba Bwana wetu ni mkuu kuliko miungu yote.

6 f Bwana hufanya lolote apendalo,
mbinguni na duniani,
katika bahari na vilindi vyake vyote.
Copyright information for SwhKC